Mahitajio
|
Utayarishaji
|
Kipimo
|
Kuku (miguu na paja)
|
Safisha, osha kwa chumvi na siki atoke harufu, chuja maji
|
12 mapande
|
Tangawizi mbichi
|
katakata, osha
|
1 kipande
|
Kitunguu saumu(thomu/galic)
|
Menya, osha
|
1 uwa zima
|
Pilipilimbichi
|
Osha
|
6
|
Pilipili mbuzi
|
Osha
|
3
|
Ukwaju
|
Roweka, kamua
|
1 kikombe cha chai
|
Bizari ya pilau/jiyra/cummin
|
1 kijiko cha chai
|
|
Bizari ya gilgilan/Dania/corriander
|
1 kijiko cha chai
|
|
Bizari ya manjano/haldi/tumeric
|
1 kijiko cha chai
|
|
Ndimu
|
kamua
|
2
|
Namna Ya Kupika:
- Chanachana (slit) mapaja ya kuku kwa ajili ya kuingiza masala.
- Katika mashine la kusagia (blender) weka tangawizi mbichi, kitunguu thomu, pilipili mbichi na mbuzi, bizari zote, chumvi na ndimu.
- Saga hadi ilainike.
- Weka kuku katika bakuli umimine mchanganyiko wa masala. Changanya vizuri kuku aingie masala kila mahahli.
- Roweka (marinate) kwa muda wa masaa mawili au zaidi, huku unageuzageuza akolee pande zote.
- Choma katika mkaa hadi aive.
- Epua kulia na saladi ya orzo
Upishi wa saladi ya Orzo unapatikana katika kiungo kifuatacho:
Kidokezo:
Unaweza kuroweka tokea usiku ukaweka katika friji, ikiwa unataka kipimo kingi kwa kuongezea vipimo vya masala.